Televisheni ya taifa ya Iran imetangaza kuwa, imethibitishwa kuwa Rais Ebrahim Rais ameaga dunia katika ajali hiyo, na tayari baraza la mawaziri linakutana kupanga taratibu za kuaga mwili wa Rais na wazaidizi wake, akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir Abdollahian aliyekuwa pamoja na Rais katika ajali hiyo.
Helikopta hiyo ilikuwa imembeba Raisi Ebrahim Raisi, Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amir-Abdollahian, Gavana wa mkoa wa Azarbaijan Mashariki Malek Rahmati, Imam wa Swala ya Ijumaa na mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu huko Tabriz, Mohammad Ali Al- Hashem na maafisa wengine kadhaa wa serikali.
342/